Faida za Mindfulness na Kutafakari Kwa Maisha Yako. Je Unajisikia kuchoka kiakili? Mawazo mengi? Au unakosa amani ya ndani?
Rafiki kama wewe ni kijana unayepitia changamoto za kila siku kama shuleni, maisha ya nyumbani, mahusiano, au hata presha ya mitandao ya kijamii basi makala hii ni kwa ajili yako! Moja ya njia rahisi na nzuri ya kutuliza akili na kuimarisha maisha yako ni kupitia mindfulness (utambuzi wa hali ya sasa) na kutafakari (meditation). Hii siyo imani au dini mazoezi ya akili na mwili ambayo kila kijana anaweza kufanya. Faida za Mindfulness na Kutafakari kwa Kijana 1. Inapunguza msongo wa mawazo (stress) Ukijifunza kutulia na kuzingatia "wakati wa uliopo", unajifunza kutoruhusu mawazo ya kukatisha tamaa au hofu ya kesho kukutawala. 2. Inasaidia kufocus Kama unajisikia unashindwa kuzingatia masomo au kazi zako, meditation inaweza kusaidia akili yako kuwa makini zaidi na kupunguza usumbufu. 3. Inaongeza furaha Mazoezi haya hukusaidia kujiangalia kwa upendo na kukubali hisia zako bila kujihukumu. Unakuwa na amani zaidi ndani yako. 4. Inakusaidia kupata usingizi mzuri Kutafakari kabla y...